Social Icons

Pages

Featured Posts

Friday, May 15, 2015

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA ULINZI LA WANANCHI TANZANIA


 
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO

Simu ya Upepo   : “N G O M E”          Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo : DSM  22150463      Sanduku la Posta 9203,
Telex                     : 41051                       DAR ES SALAAM,    15, May 2015
Tele Fax                : 2153426
Barua pepe       : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti                  : www.tpdf.mil.tz
                  
Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linasikitishwa na  taarifa za uvumi zilizotolewa  kuenea kwenye mitandao ya kijamii face book, whatsapp na twitter zikieleza kuwa JWTZ inafanya usaili leo tarehe           15 May 2015 katika Chuo cha Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) kwa wale waliosoma fani ya Computer science, IT, Electronics na Mechanical Enginering.

JWTZ linapenda kuwajulisha wananchi pamoja na watumiaji wa mitandao hiyo kuwa taarifa hizo si za kweli ni uvumi, JWTZ lina utaratibu wake wa kuandikisha Jeshini ambapo hutoa taarifa katika vyombo vya habari kwa utaratibu ulio sahihi.

   Aidha, Jeshi linaendelea kusisitiza wananchi kuwa halina akaunti za mitandao hiyo na ni kinyume cha sheria kusambaza ujumbe kwa kutumia jina au nembo ya JWTZ watakao bainika watachukuliwa hatua za kisheria dhidi yao.
   
Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.


Kwa Mawasiliano zaidi: 0783-309963.

Sunday, September 7, 2014

TAARIFA KWA UMMA: TOLEO LA SARAFU YA SHILINGI MIA TANO



Benki Kuu ya Tanzania ndiyo chombo chenye jukumu la kutoa sarafu na noti halali (legal tender) zinazotumika nchini. Katika kutekeleza jukumu hili Benki Kuu hutengeneza noti na sarafu zenye uwiano mzuri wa thamani (denominations) unaozingatia uwezekano wa zile zenye thamani kubwa kuweza kugawika katika zile zenye thamani ndogo ndogo. 

Hii hulenga kurahisisha upatikanaji wa chenji na uwezekano wa wahitaji wa viwango mbalimbali vya bidhaa na huduma  kupata katika mafungu yatakayokidhi mahitaji yao. 

Katika kutekeleza jukumu hili, Benki Kuu imetoa toleo jipya la Sarafu ya Shilingi 500. Hatua hii imezingatia yafuatayo: 
kwamba noti ya shilingi mia tano (500), ndiyo inayotumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku ya wananchi wengi kuliko noti nyingine yoyote. Hivyo noti hiyo hupita kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi sana na kuchakaa haraka. 

Noti hizi hukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila kurejeshwa kwenye mabenki kwa wakati muafaka ili zibadilishwe zinapokuwa zimefikia ukomo wake. 
Sarafu hukaa kwenye mzunguko kwa miaka mingi zaidi kuliko noti. 

Sarafu hii inatambuliwa kwa kuangalia yafuatayo:
Umbo lake ni la duara lenye michirizi pembezoni, kipenyo cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5 
Ina rangi ya fedha na imetengenezwa kwa madini aina ya chuma (Steel) na “Nickel” 
Kwa mbele ina sura ya Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Abeid Aman Karume na kwa nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.
Ina alama maalum ya usalama iitwayo “latent image” iliyopo upande wa nyuma  ambayo ni kivuli kilichojificha. Kivuli hiki huonesha thamani ya sarafu ‘500’ au neno ‘BOT’ inapogeuzwa-geuzwa.

Sarafu hii mpya ya shilingi mia tano (500) inatarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko kuanzia mwezi  Oktoba 2014.

Sarafu hii, itakuwa ikitumika sambamba na noti zilizopo sasa za shilingi mia tano mpaka hapo noti hizo zitakapokwisha katika mzunguko. 

Pamoja na taarifa hii; tunawaomba wananchi kuendelea kufuatilia vipindi mbalimbali vitakavyokuwa vinaeleza jinsi sarafu hii ilivyo na namna ya kutunza noti na sarafu zetu kwa njia salama.

Ahsanteni Sana

Thursday, April 3, 2014

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI KUTOKA SECRETARIETI YA AJIRA UTUMISHI WA UMMA



Kwa lugha ya Kiswahili


KAMA UNATAKA KUTIZAMA NAFASI HIZI KWA KUGHA YA KIINGEREZA BASI BOFYA HAPA CHINI

TAARIFA YA KUFUNGWA KWA BARABARA YA BAGAMOYO - MAKOFIA - MSATA KUTOKANA NA MAFURIKO


MTENDAJI MKUU WA WAKALA WA BARABARA TANZANIA (TANROADS) ANAPENDA KUTOA TAARIFA KWA  UMMA NA WATUMIA BARABARA YA BAGAMOYO – MAKOFIA - MSATA KWAMBA BARABARA HII IMEFUNGWA KWA AJILI YA USALAMA  WA ABIRIA NA VYOMBO VYA USAFIRI KUTOKANA NA MVUA KUBWA ZINAZONYESHA NCHINI NA KULETA MAFURIKO KWENYE BONDE LA DARAJA LA RUVU CHINI.

MADEREVA WANASHAURIWA KUTUMIA BARABARA YA DAR ES SALAAM – CHALINZE - MOROGORO NA BAGAMOYO – MLANDIZI – CHALINZE KWA KIPINDI HIKI AMBACHO BARABARA YA BAGAMOYO – MAKOFIA – MSATA IMEFUNGWA. 

TUNAOMBA RADHI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA NA ASANTE KWA USHIRIKIANO.

IMETOLEWA NA,
MTENDAJI MKUU – WAKALA WA BARABARA
P.O BOX 11364
3RD FLOOR
AIRTEL  BUILDING
ALI HASSAN MWINYI/ KAWAWA ROADS JUNCTION
DAR ES SALAAM

Tuesday, April 1, 2014

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU ZIARA YA RAIS KIKWETE NCHINI UINGEREZA

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
       P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
                                                                                      
TAARIFA KWA UMMA

Uingereza inajivunia kuwa nchi inayoongoza katika uwekezaji nchini Tanzania na itaendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada zake za kiuchumi na kuleta maendeleo .

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amemuambia Rais Kikwete wakati wa mazungumzo yaliyofanyika 10 Downing Street,  Leo tarehe 31 March, 14, ambapo ndipo yalipo Makao Makuu ya Waziri Mkuu wa Uingereza.

"Tunafurahia sana uhusiano wetu na kujivunia kuwa tunaongoza katika
Uwekezaji nchini Tanzania" Bw. Cameron amesema na kumhakikishia Rais Kikwete kuwa Uingereza iko tayari kutoa misaada zaidi.

Rais Kikwete amewasili nchini Uingereza tarehe 30 Machi, 2014 kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku 3 kufuatia mualiko wa Bw. Cameroon ambaye pia amemuomba Rais Kikwete aendelee kutoa mchango wake wa mawazo katika masuala ya kimataifa hasa baada ya mwisho wa muda wa malengo ya millennium ya 2015.

"Tunakaribia mwisho wa muda wa malengo ya millennia Mwaka 2015, tutahitaji kuweka vipaumbele vingine baada ya hivyo kama kuondosha umaskini, Maji safi na salama, masuala ya ufisadi na utawala bora, natumaini utaendelea kutoa mchango wako baada ya malengo hayo kufikia tamati" Waziri Mkuu Cameron amemuambia Rais Kikwete ambapo Rais amekubali ombi hilo na kuahidi ushirikiano wake.

Mapema leo asubuhi Rais amekutana na mtoto wa Mfalme Prince Andrew katika makazi ya Malkia ya Buckingham ambapo wamebadilishana mawazo kuhusu mambo mbalimbali ya Kimataifa na Kijamii.

Kabla ya kwenda Buckingham Rais amefungua mkutano kuhusu uwekezaji na kuelezea fursa na nafasi zilizopo za uwekezaji nchini Tanzania na kuelezea kwanini wawekezaji watakuwa wanafanya uamuzi bora kwa kuwekeza Tanzania kuwa ni pamoja na;

"Fursa nyingi, amani, usalama, soko la kutosha na kubwa kwa vile Tanzania iko katika Umoja wa Afrika Mashariki, Ukanda wa Maziwa Makuu na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika,hivyo kuwa na uhakika wa soko kubwa na pana" amesema.

Katika ziara yake Rais pia amekutana na Mstahiki Meya  wa Jiji la London Mama Alderman Fiona Woolf na kukaribishwa rasmi Jijini London. Mstahiki Meya  anatarajia kutembelea Tanzania, Mwezi Septemba Mwaka huu.

Rais alipowasili London tarehe 30 Machi,2014, alikutana na Watanzania wanaoishi nchini Uingereza na kuwaeleza maendeleo yaliyopo nchini Tanzania.

Rais anaendelea na ziara yake nchini Uingereza

Mwisho.

Imetolewa na;

Premi Kibanga.
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
London Uingereza
31 Machi, 14

Monday, February 10, 2014

TAARIFA YA WIZARA YA MAMBO YA NJE KUHUSU WAFUNGWA WA KITANZANIA NCHINI CHINA



Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inapenda kukanusha taarifa za uvumi zinazosambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na vyombo vya habari kuwa kuna Watanzania wapatao 160 wamenyongwa nchini China kwa kosa la kusafirisha madawa ya kulevya.
Wizara inapenda kuujulisha Umma kuwa hakuna Mtanzania yeyote aliyenyongwa kama inavyodaiwa kwenye mitandao na vyombo vya habari.
Aidha, taarifa hiyo ya uvumi imedai kuwa ndugu wa mmoja wa Watanzania hao ambaye kwa jina anajulikana kama Bw. Rajab Mohamed Ismail Mapusa wamekaa matanga kuomboleza kifo chake.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Serikali ya China, Bw. Mapusa yupo hai gerezani akitumikia kifungo cha maisha kwa kosa la kuingiza madawa ya kulevya nchini humo, na hivi karibuni alishiriki kuandaa maonyesho ya utamaduni wa Kiafrika wakati wa kuadhimisha sherehe za Mwaka Mpya wa China.
Wizara inapenda kuwakumbusha Wanahabari kuandika taarifa ambazo ni sahihi zisizopotosha Umma kwa kuzingatia weledi, maadili na ukweli kutoka mamlaka zote husika.
Imetolewa na: Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam
10 Februari, 2014

 

Sample text

Sample Text

Sample Text